Saturday, March 31, 2007

Mrema amcharukia Tao kwa madai ya Mahakama

Na Aisha Mbaga

MWENYEKITI wa Chama Cha Tanzania Labour (TLP) Agustine Mrema, amesema amekanusha taarifa za kuwa amezuiwa na Mahakama Kuu kufanya shughuli za chama wala kutumia fedha kama inavyoelezwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Hamadi Tao.

Kauli hiyo ya Mrema, imetokana na taarifa ya Tao, ambayo ambayo amelieleza Tanzania Daima kwamba mahakama imetia uamuzi wa kumzuia Mrema asijiusishe na kazi za chama wala kutumia fedha za chama hicho.

Akizungumza kwa njia ya simu jana Mrema, alisema kuwa, yeye hajashindwa kesi na pia hajapewa barua ya kufungiwa kwa chama chake na kuzuiwa kuitisha kikao cha kamati kuu ya chama hicho.

Mrema alisema kuwa, yaliyopo mahakamani ni malalamiko na kila mtu ana uhuru wa kwenda Mahakamani kupeleka malalamiko yake na akasikilizwa hivyo Tao anahaki hiyo asubiri maamuzi ya Mahakama yatakaposikiliza lalamiko lake.

Pia alisema kuwa,TLP kwa sasa haimtambui Tao kuwa ni mwanachama wa chama hicho kwakuwa Kikao cha Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya chama hicho kilimfukuza uanachama yeye na wenzake 23 baada ya kubainika kuwa ni waasi wa chama hicho.

"Siwezi kuacha kuendelea na shughuli za chama changu kwa kuwa sijapewa barua ya kusimamisha shughuli na TLP bado haijavunjwa, pesa tunazotumia ni kwaajili ya shughuli za chama na katiba yetu inaturuhusu kutumia pesa za chama kwa shughuli za chama,"alisisitiza Mrema.

"Ndugu Mwandishi huyo Tao,kuwa nae makini kwakuwa ana kila dalili za kuchanganyikiwa akili kwakuwa ni yeye mwenyewe ndiye aliyeenda kufungua Mahakama Kuu,akipinga kufukuzwa uanachama, sasa mahakama bado haijatoa uamuzi.....yeye ameishaanza kupita kwenye vyombo vya habari kuwaletea habari za uongo ambazo msipokuwa makini naye mkazichapisha gazeti letu litaishia kushitakiwa kwaajili yake",alisema Mrema.

"Tao nakwambia usinifuate futae, mimi siyo saizi yako, tulia nyumbani kwako usubiri mahakama itatoa uamuzi gani kwenye kesi iliyofungua....kwanza kitendo hichi unacho kifanya ni kinyume na sheria kwakuwa mahakama bado haijatoa uamuzi wewe unapita kwenye vyombo vya habari kusema bahari za uongo ambazo mahakama haijazisema na sema hivi mchezo huo unaidharirisha mahakama yetu ambayo tunaimani nayo." alisema Mrema.

Hata hivyo Mrema aliviomba vyombo vyote vya habari kuwa makini na Tao, kwakuwa amekuwa akitoa taarifa za uongo kuhusu shauri lililopo mahakamani kuwa limeishatolewa uamuzi jambo ambalo si kweli.

Mrema alisema hawatishiki na kauli za Tao na kusema kuwa TLP itaendelea na shughuli za kichama kama kawaida kwakuwa ni moja ya haki za msingi ya chama hicho na kuongeza kuwa April 3,mwaka huu, chama chake kitafanya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF, Professa Ibrahim Lipumba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Mapema jana asubuhi aliyekuwa Katibu wa chama hicho Hamadi Tao, alitembelea ofisi za gazeti hili alisema Mahakama Kuu,imezuia vikao vya TLP hadi itakapotoa maamuzi lakini ameshangazwa na kitendo cha Mrema kuitisha kikao cha kamati kuu bila kuwashirikisha.

Tao alisema kuwa, kutokana na kufukuzwa uanachama wa TLP walifungua kesi Mahakama Kuu wakidai fidia ya Milioni tano na kutaka kusimamisha kwa shughuli zote za chama hadi Mrema kutokana na ubadhirifu wa fedha za chama hicho unaofanywa na Mrema kwa manufaa yake mwenyewe.

Alisema kuwa, pia wamefungua kesi nyingine katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakiomba kukaguliwa kwa mahesabu ya TLP na wakaguzi wa serikali ili kubainisha matumizi sahihi ya chama hicho.

Tao aliongeza kuwa, Katika kesi iliyopo Mahakama Kuu namba 138 ya mwaka 2006, wanaiomba Mahakama pia iwarudishie uongozi wao na kutambuliwa kama wanachama halali wa chama hicho na kesi ya Kisutu wanaiomba Mahakama isimamishe shughuli zote za chama hicho ikiwa ni pamoja na kuzuia matumizi ya fedha za chama hicho.

Mwisho.
Na Aisha Mbaga

Mpenzi msomaji wa safu hii nakukaribisha tena uungane nami katika chumba changu hiki cha mahaba tuweze kujimwayamwaya na kujinafasi kwa raha zetu.Wiki uliyopita tulikuwa tukizungunzia udhaifu wa wanaume katika suaka zima la mapenzi na sababu zinazopelekea wao kuwa katika hali hiyo.tilibaini kuwa kwa upande mwingine wanakuwa na usongo wa kutimiza lengo hivyo wanapofika katika mchezo wakajikuta wameshindwa kuukwea mnazi, upande mwingine ni maumbile ya kibaiolojia na upande mwingine wanawale tunachangia kwa kutokuwa makini ama kujihusisha na mapenzi kwa wakati.leo nataka kuueleza jinsi wanawake walivyo wezi wa mabwana wa mashoga zao na jinsi wanavyoweza kusambaratisa penzi lililoota mizizi.
mwanamke anapotaka kukufanyia unyama kwa mpenzio hashindwi haswa pale unapokuwa umemweka karibu na mpenzio.kila mwanamke huwa na shoga na wengine hupenda kusema mambo ya kweli wanayoyapenda wapenzi wao na kumpa nafasi kubwa rafiki yake pale anapotaka kuporomosha penzi hilo.mwanamke anamitego mingi kwa mwanaume ikia i pamoja na kumpelekea zawadi ambazo mpenzi wake hampi.kumfanyia mambo ya mahaba ambayo hayapati kwa mpenzi wake na kisha kumtega kwa vivazi, na urembo wa asili. kina mavazi ambayo yamnamvutia mwanaume apende asipende, atatamani kuwa na wewe, mavazi haya si lazima yawe mini sket au top na pedo, waweza vaa hata baibui lakii kutokana na jinsi lilivyo likamvutia mwanaume na kujikuta anashindwa kujizuia na kuingia katika mtego wa mhaba mazito ambayo anadhani kuwa atayapatantoka kwako. kinachosababisha matatizo haya ni kutokana na kuaminiana kwa hali ya juu kati ya mashoga hawa na kuambiana siri zao za ndani juu ya wapenzi wao. ukweli ni kwamba, usipende kumweleza rafii yako mambo ya anayokufanyia mpenzio kwani unampa nafasi ya kuweza kumteka hususani anapojua kuwa mpenzio anaudhaifu gani. kama kunaulazima wa kuhadithiana juu ya wapenzi wenu, kuwa makini na wakati mwingine ni heri umwambia rafukiyo uongo ili kuweza kulinda penzi kwani kikulacho kinguoni kwako. wanawake wengi hawapendi kuona mwenzao kafanikiwa, ama kuona penzi la mtu likiwa imara, ni dhahiri kuwa wapo wanaochukia na kutafuta mbinu za kuliporomosha hata wakishindwa wao watatumia watu wa pembeni yenu bila ya wewe kujua kuwa shoga, rafikiyo mkubwa anakugeuka na kukuzunguka. waweza kusema sitaki kuwa na rafiki mwanamke kutokana na tabia za baadhi yao kuwa za unafiki na wivu kwa maendeleo ya mtu. kama ujuavyo mapenzi ni makubaliano kati ya watu wawili na yanaweza kuvunika muda wowote endapo wanaweza kushindana na kutofikia malengo. hilo si jambo la ajabu kwani ndio maana hata leo tunaweza kuona kwenye baadhi ya michezo ya tamthilia watu wakiamua kutalikiana ili kila mtu aishi kwa amani. ni mara chache sana waweza kumuona mwanake anasikitika kwa kuona penzi la mtu likiishia mitini hususan pale watu hawa wanapokuwa wachumba ama ndio kwanza wanaanza, achilia mbali waliooana na kuchokana. wanawake wengi wako makini kuhakikisha kuwa ndoa ya mtu fulani haifungwi na kufanikiwa kuvunja uchumba wa wawili hawa na wakati mwingine ndo kwanza maapenzi yanaanza lakini yataingiliwa na kidudu mtu na kuharibiwa. yote haya ni kutokana na mashoga na chanzo ni kupeana siri za wachumba wenu. tuweni makini na tuache kuaminiana kwani umwaminiye ndiye adui yako.

napenda kuwashukuru wasomaji wangu walionipigia simu na kunipongeza na pia kunipa ushauri, nakarubisha maoni yenu kwangu na nitayafanyia kazi bila kusita. pia napenda kumpa pole mama yangu ambaye aliniambia kuwa mumewe amekuwa kicheche kwa kutembea na watoto wadogo anaoweza kuwazaa bila kujali walipotoka na uzee walionao. napenda kumshauri mama huyu kutoka Tabata jijini Dar es Salaam kuwa asijali kuona mumee kamsaliti kwani hiyo ni kawaida ya wanaume wengi ila lamsingi namshauri amwombe wakapime afya zao kulingana na hali tuliyonayo.

kwa maoni na ushauri wasiliana nami kwa simu namba 0755-690690 au kwa barua pepe aishamudysaan@yahoo.com
Na Aisha Mbaga
MWENYEKITI wa Chama Cha Tanzania Labour (TLP) Agustine Mrema, amesema amekanusha taarifa za kuwa amezuiwa na Mahakama Kuu kufanya shughuli za chama wala kutumia fedha kama inavyoelezwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Hamadi Tao.
Kauli hiyo ya Mrema, imetokana na taarifa ya Tao, ambayo ambayo amelieleza Tanzania Daima kwamba mahakama imetia uamuzi wa kumzuia Mrema asijiusishe na kazi za chama wala kutumia fedha za chama hicho.
Akizungumza kwa njia ya simu jana Mrema, alisema kuwa, yeye hajashindwa kesi na pia hajapewa barua ya kufungiwa kwa chama chake na kuzuiwa kuitisha kikao cha kamati kuu ya chama hicho.
Mrema alisema kuwa, yaliyopo mahakamani ni malalamiko na kila mtu ana uhuru wa kwenda Mahakamani kupeleka malalamiko yake na akasikilizwa hivyo Tao anahaki hiyo asubiri maamuzi ya Mahakama yatakaposikiliza lalamiko lake.
Pia alisema kuwa,TLP kwa sasa haimtambui Tao kuwa ni mwanachama wa chama hicho kwakuwa Kikao cha Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya chama hicho kilimfukuza uanachama yeye na wenzake 23 baada ya kubainika kuwa ni waasi wa chama hicho.
"Siwezi kuacha kuendelea na shughuli za chama changu kwa kuwa sijapewa barua ya kusimamisha shughuli na TLP bado haijavunjwa, pesa tunazotumia ni kwaajili ya shughuli za chama na katiba yetu inaturuhusu kutumia pesa za chama kwa shughuli za chama.
"Ndugu Mwandishi huyo Tao,kuwa nae makini kwakuwa ana kila dalili za kuchanganyikiwa akili kwakuwa ni yeye mwenyewe ndiye aliyeenda kufungua Mahakama Kuu,akipinga kufukuzwa uanachama, sasa mahakama bado haijatoa uamuzi.....yeye ameishaanza kupita kwenye vyombo vya habari kuwaletea habari za uongo ambazo msipokuwa makini naye mkazichapisha gazeti letu litaishia kushitakiwa kwaajili yake.
"Tao nakwambia usinifuate futae, mimi siyo saizi yako, tulia nyumbani kwako usubiri mahakama itatoa uamuzi gani kwenye kesi iliyofungua....kwanza kitendo hichi unacho kifanya ni kinyume na sheria kwakuwa mahakama bado haijatoa uamuzi wewe unapita kwenye vyombo vya habari kusema bahari za uongo ambazo mahakama haijazisema na sema hivi mchezo huo unaidharirisha mahakama yetu ambayo tunaimani nayo." alisema Mrema.
Hata hivyo Mrema aliviomba vyombo vyote vya habari kuwa makini na Tao, kwakuwa amekuwa akitoa taarifa za uongo kuhusu shauri lililopo mahakamani kuwa limeishatolewa uamuzi jambo ambalo si kweli.
Mrema alisema hawatishiki na kauli za Tao na kusema kuwa TLP itaendelea na shughuli za kichama kama kawaida kwakuwa ni moja ya haki za msingi ya chama hicho na kuongeza kuwa April 3,mwaka huu, chama chake kitafanya kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF, Professa Ibrahim Lipumba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Mapema jana asubuhi aliyekuwa Katibu wa chama hicho Hamadi Tao, alitembelea ofisi za gazeti hili alisema Mahakama Kuu,imezuia vikao vya TLP hadi itakapotoa maamuzi lakini ameshangazwa na kitendo cha Mrema kuitisha kikao cha kamati kuu bila kuwashirikisha.
Tao alisema kuwa, kutokana na kufukuzwa uanachama wa TLP walifungua kesi Mahakama Kuu wakidai fidia ya Milioni tano na kutaka kusimamisha kwa shughuli zote za chama hadi Mrema kutokana na ubadhirifu wa fedha za chama hicho unaofanywa na Mrema kwa manufaa yake mwenyewe.
Alisema kuwa, pia wamefungua kesi nyingine katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakiomba kukaguliwa kwa mahesabu ya TLP na wakaguzi wa serikali ili kubainisha matumizi sahihi ya chama hicho.
Tao aliongeza kuwa, Katika kesi iliyopo Mahakama Kuu namba 138 ya mwaka 2006, wanaiomba Mahakama pia iwarudishie uongozi wao na kutambuliwa kama wanachama halali wa chama hicho na kesi ya Kisutu wanaiomba Mahakama isimamishe shughuli zote za chama hicho ikiwa ni pamoja na kuzuia matumizi ya fedha za chama hicho.

Mwisho.

Thursday, March 29, 2007

Utalii; Kitovu cha Maendeleo
Visiwa hivi vya marashi ya Karafuu, ni maarufu kwa fukwe zake maridadi, matumbawe
na mji wenyewe wa kihistoria; Mji Mkongwe. Kwa maana hiyo, utalii ni sekta muhimu
katika uchumi wa Zanzibar na huchangia asilimia 26 kwa pato la taifa na uchangiaji huo
unatarajiwa kukua kwa kati ya asilimia 5 na 10 kwa mwaka.
Manispaa ya Zanzibar ni injini muhimu zaidi katika sekta ya utalii. Mji huu ndio lango
kubwa la watalii, achilia mbali wenyewe kuwa kivutio. Kabla ya watalii kwenda pwani ya
mashariki, kwa kawaida hukaa kwa muda katika Mji Mkongwe kufurahia mandhari yake
(tazama ramani 2.1)
Moja Ya Sehemu Za Ufukwe Kisiwani Zanzibar
Mitaa myembamba ya mji huu, hali ya hewa iliyotulia, majengo ya kale, milangu
inayopendeza iliyochongwa kwa mtindo wa aina yake ya kuviringwa, maegesho na
fukwe ndivyo vitu vinavyowavutia zaidi watalii hapa. Mji huu Mkongwe unazo hoteli
nyingi, migahawa na maduka kwa watalii ambayo pia hutoa ajira kwa watu kutoka
Unguja, Pemba na hata Tanzania Bara.
Idadi ya hoteli zenye hadhi za kulaza wageni imeongezeka kwa kiasi kikubwa katika
kipindi cha miaka mitano iliyopita. Hata hivyo, hakuna uhakika wa hasa ni hoteli ngapi
zinazolaza watalii mjini hapa. Makadirio mengi yanaonyesha kwamba kuna vyumba
karibu 20,000 vya kulala kote kisiwani, na takriban asilimia 50 ya hizo, iko mjini.
Kamisheni ya Utalii ilirekodi ongezeko la asilimia 25 ya vyumba vinavyokodishwa kwa
watalii tangu mwaka 1987 hadi 1997. Jumla ya watalii walirekodiwa kuingia uwanja wa
ndege na kwenye bandari mbalimbali katika kipindi hicho, ni 587,640.
Sera ya Utalii Zanzibar imekuwa ikiegemea katika falsafa ya ubora wa hali ya juu na ujazo
mdogo wa watalii, mambo yanayoleta mapato makubwa kiuchumi kutoka kwenye sekta
hiyo, kwa ajili ya watu ambao ni wengi kisiwani, huku kukiwa na rasilimali chache.
Mwaka 1997, zaidi ya watalii 86,000 walitembelea Zanzibar wakati mwaka 1998, zaidi ya
watalii 100,000 walitarajiwa (tazama chati juu ya idadi ya watalii).
Japokuwa majengo ya kale hayapo Mji Mkongwe pekee, umaarufu wake unatokana
zaidi na kuwa mji wa kihistoria ambao pia ni makazi, ukiwa na majengo yenye
kupendeza, milango ya aina yake iliyoviringwa juu na kurembwa vilivyo, mitaa
myembamba ambayo watalii huishangaa na kufurahia sambamba na maisha ya jumla ya
Zanzibar.
Kivutio kingine kwa watalii ni rasilimali za bahari zilizopo. Ni kweli kwamba fukwe
zilizoko ndani ya Manispaa ya Zanzibar ni chache, visiwa vilivyo mbele ya mji, vina
matumbawe ya kupendeza ambayo ni maridhawa kwa ajili ya kuzamia na hata kupiga
mbizi. Uvuvi Kisiwani Zanzibar na Tabia Zake
Mazingira ya uvuvi Zanzibar ni ya kupendeza na inakadiriwa kwamba mwaka 1997, kiasi
cha watu 12,000 walirekodiwa kama wavuvi na vyombo vya uvuvi vilivyokuwepo wakati
huo ni 2,700.
Idadi kubwa ya watu (kwa mfano mwaka 1990, watu 6,000 kwa Pemba na Unguja),
hufanya kazi hutoa huduma katika sekta hii na huduma zihusianazo. Asilimia 22 ya
bajeti za kaya hutumika kununua samaki ambao ni chanzo kikubwa cha protini
Zanzibar, hasa kwa wale wenye kipato kidogo.
Manispaa ya Zanzibar ina vituo tisa vya kuvulia samaki ambavyo ni Malindi,
Malindi/jetty, Kizingo, Forodhani, Maruhubi, Kilimani, Mtoni, Mazizini na Bububu
(tazama ramani 2.3). Wastani wa samaki wanaovuliwa baharini katika maeneo ya Unguja
na kuletwa Manispaa ya Zanzibar ni takriban tani 2,273 kwa mwaka. Idadi ya samaki
wanaovuliwa kote Zanzibar ni kati ya tani 10,000 hadi 20,000 kwa mwaka na hii ni kwa
mujibu wa utafiti uliofanywa na Kamisheni ya Ardhi na Mazingira.
Wavuvi wenyeji hutumia karibu asilimia 96 ya samaki wanaowavua kwa soko la hapa
hapa, na wanaouzwa nje ni asilimia 4 tu. Kwa sasa, Manispaa ya Zanzibar ina kampuni
moja tu ya uvuvi iliyosajiliwa, yenyewe ikijulikana kama ZAFFICO. Ina waajiriwa wa
kudumu 60.
Wavuvi wengi wana vifaa duni na ndio sababu hasa ya uchache wa samaki wanaovuliwa.
Japokuwa takwimu zilizopo na za kuaminika hazitoshi, kuna vyanzo vinavyoonyesha
kwamba jumla ya idadi ya samaki waliopo kwenye maeneo haya, inapungua.

Uvuvi katika Manispaa ya Zanzibar unahusisha wale wavuvi wa asili na wengine ambao
wamekuja kufanya hivyo baadaye kwa sababu za kibiashara. Hawa wa asili,
wanaoonekana kama wasanii, hutumia vyombo vya uvuvi vya kijadi na mbinu za
kizamani, tofauti na wale wa kisasa ambao hutumia boti au vifaa vyenye injini.
Hawa wa asili huweza pia kutumia mishipi au fito na huweza kupata samaki wa
miambani na wa maji wazi kama kingfish na tuna. Wale wavuaji wa kibiashara zaidi
hupata samaki wa jamii ya bangala na wengine wadogo wadogo.
Samaki walioletwa Manispaa ya Zanzibar na kiasi chake kwa tani, thamani ikiwa katika
milioni za shilingiUchimbaji Zanzibar ni wa aina ndogo, ukilenga zaidi katika mchanga, mawe,
changarawe, chokaa na mchanga wa fukweni. Maeneo haya ya machimbo ni ya saizi
ndogo na ya kati na yamesambaa maeneo mbalimbali kisiwani.
Maeneo rasmi ya machimbo ni machache nje ya mipaka mipya ya mji, mmoja ukiwa ni
wa mchanga, katika eneo lenye ukubwa wa hekta mbili kwenye Wilaya ya Kaskazini B
na mengine mawili ya uchimbaji mawe na eneo moja la uchimbaji chokaa Wilaya ya
Magharibi. Mjini hakuna eneo rasmi la machimbo lakini hayo yaliyopo nje, hutumika
kwa ajili ya mji huu kwani inakadiriwa kwamba asilimia 90 ya yanayochimbwa huletwa
mjini.
Bidhaa hizo hutumika zaidi kwa ajili ya shughuli za ujenzi. Kuna maeneo mengine mengi
yasiyo rasmi, hasa kwa ajili ya kuchimba mchanga na ambayo hutumiwa ndani ya
manispaa, hasa katika maeneo jirani. Mchanga unachimbwa pia kinyume cha sheria
kwenye maeneo kama Mpiga Duri, Daraja Bovu, Amani, Welezo na Mpendae na
maeneo mengine kwenye kingo za mito. Ni vigumu kudhibiti hali hii kwani wachimbaji
hufanya kazi hiyo usiku. Jasi na udongo huchimbwa Mtoni, Chumbuni na Magogoni.
Ni kawaida kuona ngamia au ng’ombe dume wakibeba nyenzo hiyo vya ujenzi. Maeneo
yaliyoathirika zaidi ni Amaani, Magogoni na Maruhubi. Vitendo hivyo visivyo rasmi na
visivyoratibiwa katika Manispaa ya Zanzibar, vilisababisha mjadala mkali kwenye Baraza
la Wawakilishi kutokana na mmomonyoko wa ardhi. Japokuwa ilikubaliwa wizara husika
ichukue hatua, hali imebaki kuwa hivyo hivyo
Kilimo kimekuwa daima na umuhimu mkubwa kwa uchumi wa Zanzibar. Siku
zilizopita, uchumi ulitegemea kwa kiasi kikubwa mauzo ya karafuu na nazi nje ya nchi.
Hata hivyo, kupungua kwa bei kwenye masoko, kunaathiri kwa kiasi kikubwa mazao
hayo.
Katika Manispaa ya Zanzibar, kilimo kina mguso kidogo katika maendeleo ya mji.
Kilimo cha mjini ni kidogo, kama bustani tu na wajibu wa mji huu katika kilimo, ni kwa
vile tu mji huu ni soko kubwa kwa bidhaa za kilimo. Katika Mji Mkongwe hapafanyiki
kilimo, bali kinafanyika maeneo ya Ng’ambo lakini nako, kilimo kinashuka.
Maeneo ambayo kilimo kinafanyika zaidi ni Kilimani, Maruhubi, Saateni, Migombani -
Kaburi Kikombe, Kwaalinatu - Ziwani, Chumbuni, Mtoni, Kwahani na Sebleni, maeneo
yenye kiasi cha hekta 95. Mengi ya maeneo haya huzalisha chakula na mengine
yamegeuka kuwa mabwawa, hasa nyakati za mvua. Mpunga ndio zao kubwa linalolimwa
huko, likifuatiwa na ndizi na mboga kama vile spinachi, kabichi na nyinginezo. Katika
maeneo makavu kisiwani, viazi vitamu na mihogo hulimwa pia.
Maeneo haya yanatambuliwa rasmi na Wizara ya Kilimo, na wakazi hujitahidi kupanda,
japo miti michache ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao. Wengi wanaojihusisha
na kilimo cha mjini ni wanawake.
Mifugo kisiwani ipo pia, nayo ni kama ng’ombe, mbuzi, kuku, ngamia, bata na paka
ambao hupatikana maeneo ya Ng’ambo. Kuku na bata ndio wapo kwa wingi,
wakifuatiwa na ng’ombe na mbuzi. Maeneo ya Ng’ambo yenye mifugo mingi zaidi ni
Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe, Mtoni, Bububu. Chukwani na Chumbuni.
Kwa sasa, mifugo katika kisiwa chote, huchangia asilimia 12 ya pato la taifa. Kuna
mipango ya kuboresha zaidi sekta hii ili kupunguza utapiamlo na pia kufikia mahitaji
halisi kwa wakazi wa mjini na sekta ya utalii. Kwa mujibu wa sensa ya mifugo ya mwaka
1993, kuna mifugo 73,000 katika visiwa vya Pemba na Unguja na kati ya hiyo, 13,000
ipo Wilaya za Mjini na Magharibi.
Katika maeneo ya kingo za mji, kwenye udongo wenye rutuba kwa ajili ya kilimo, ardhi
inagombewa kwa sababu mji nao unapanuka. Mashariki mwa mji, hasa maeneo
yaliyokuwa yakitumiwa kwa kilimo awali, sasa yanalazimika kuendelezwa kwa makazi.
Hali hii hupunguza maeneo ya uzalishaji chakula lakini pia husababisha mmonyoko wa
ardhi.
Kilimo kimekuwa daima na umuhimu mkubwa kwa uchumi wa Zanzibar. Siku zilizopita,
uchumi ulitegemea kwa kiasi kikubwa mauzo ya karafuu na nazi nje ya nchi. Hata hivyo,
kupungua kwa bei kwenye masoko, kunaathiri kwa kiasi kikubwa mazao hayo.
Katika Manispaa ya Zanzibar, kilimo kina mguso kidogo katika maendeleo ya mji.
Kilimo cha mjini ni kidogo, kama bustani tu na wajibu wa mji huu katika kilimo, ni kwa
vile tu mji huu ni soko kubwa kwa bidhaa za kilimo. Katika Mji Mkongwe hapafanyiki
kilimo, bali kinafanyika maeneo ya Ng’ambo lakini nako, kilimo kinashuka.
Maeneo ambayo kilimo kinafanyika zaidi ni Kilimani, Maruhubi, Saateni, Migombani -
Kaburi Kikombe, Kwaalinatu - Ziwani, Chumbuni, Mtoni, Kwahani na Sebleni, maeneo
yenye kiasi cha hekta 95. Mengi ya maeneo haya huzalisha chakula na mengine
yamegeuka kuwa mabwawa, hasa nyakati za mvua. Mpunga ndio zao kubwa linalolimwa
huko, likifuatiwa na ndizi na mboga kama vile spinachi, kabichi na nyinginezo. Katika
maeneo makavu kisiwani, viazi vitamu na mihogo hulimwa pia.
Maeneo haya yanatambuliwa rasmi na Wizara ya Kilimo, na wakazi hujitahidi kupanda,
japo miti michache ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao. Wengi wanaojihusisha
na kilimo cha mjini ni wanawake.
Mifugo kisiwani ipo pia, nayo ni kama ng’ombe, mbuzi, kuku, ngamia, bata na paka
ambao hupatikana maeneo ya Ng’ambo. Kuku na bata ndio wapo kwa wingi,
wakifuatiwa na ng’ombe na mbuzi. Maeneo ya Ng’ambo yenye mifugo mingi zaidi ni
Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe, Mtoni, Bububu. Chukwani na Chumbuni.
Kwa sasa, mifugo katika kisiwa chote, huchangia asilimia 12 ya pato la taifa. Kuna
mipango ya kuboresha zaidi sekta hii ili kupunguza utapiamlo na pia kufikia mahitaji
halisi kwa wakazi wa mjini na sekta ya utalii. Kwa mujibu wa sensa ya mifugo ya mwaka
1993, kuna mifugo 73,000 katika visiwa vya Pemba na Unguja na kati ya hiyo, 13,000
ipo Wilaya za Mjini na Magharibi.
Katika maeneo ya kingo za mji, kwenye udongo wenye rutuba kwa ajili ya kilimo, ardhi
inagombewa kwa sababu mji nao unapanuka. Mashariki mwa mji, hasa maeneo
yaliyokuwa yakitumiwa kwa kilimo awali, sasa yanalazimika kuendelezwa kwa makazi.
Hali hii hupunguza maeneo ya uzalishaji chakula lakini pia husababisha mmonyoko wa
ardhi.
mwisho
Usultani Hadi Taifa Huru

Manispaa ya Zanzibar imegawanyika kihistoria katika maeneo mawili, nayo ni Mji Mkongwe na

Ng’ambo. Kuibuka na kukua kwa maeneo haya tangu karne ya 19, kumekuwa katika misingi ya

kiuchumi. Mji Mkongwe uliojengeka vema, ulikuwa kwa ajili ya matajiri na wasomi wakati viunga vya

Ng’ambo, vikawa kwa ajili ya walalahoi.

Mji Mkongwe ulianza kukua taratibu, awali kama makazi ya wavuvi kwenye Rasi ya Shangani katika

karne ya 12. Ulikuwa mji wa Kiswahili hasa, baadhi ya watu wakijishughulisha na sanaa za mikono, na

ikawa sehemu ya biashara zile ndefu zilizofanywa kwa njia ya bahari.

Kunako karne ya 17, Malkia Fatima alipotawala Unguja ya Kati, Mji wa Zanzibar uligeuka na kuwa

makao makuu ya falme yake. Alirithiwa na mwanawe Hasan, anayesemekana alifanya mengi katika

ujenzi wa Mji Mkongwe. Kuingia kwa wafanyabiashara wa Kireno pamoja na wale wa Kiarabu mwaka

1822, kulisababisha Waswahili kuhamia pande za mashariki mwa Mji Mkongwe.

Utawala wa Wareno ulipoanza kusambaratika katika Afrika Mashariki, Waarabu wa Oman, ambao awali

walikuja kama wafanyabiashara, walitwaa madaraka kisiwani Zanzibar. Waligeuza uchumi wa Zanzibar

kutegemea zaidi kilimo cha mashamba makubwa, ndipo uzalishaji wa karafuu ukashamiri na kukipatia

kisiwa umaarufu mkubwa. Japokuwa wamiliki ardhi hiyo walijenga nyumba mashambani, watu wengi

walipendelea zaidi makasri kandokando ya bahari, karibu na hekalu la Sultani.

Eneo ulipokuwa mji wa Zanzibar, lilikuwa jambo la umuhimu mkubwa, hasa wakati Sultani wa Oman,

Seyyid Said alipokuja Zanzibar na akaamua kuufanya kuwa makao makuu. Iliripotiwa kwamba idadi ya

watu kwenye mji huo ilikuwa kati ya 10,000 na 12,000.

Ujio wa Sultani Seyyid Said, ulileta zama mpya kwani mji huo uligeuka kuwa kituo kikuu cha biashara

katika Pwani ya Mashariki mwa Afrika. Misafara ya kibiashara ilistawi kwa kiasi kikubwa na yenye faida

pia, ikihusisha uuzaji watumwa kutoka pwani hii. Watumwa hao walitumiwa kuzalisha bidhaa

mbalimbali pamoja na dhahabu. Biashara ilistawi na misururu kutoka bara, ilileta pembe za ndovu,

dhahabu na watumwa ambao walifanya kazi kwenye mashamba hayo makubwa.

Ni mtawala huyo huyo ambaye aliweka misingi ya kuendeleza mji huu na pia, licha ya karafuu, mazao

mengine yaliyozalishwa kwa kiasi kikubwa ni minazi. Uzalishaji wa mazao haya ya biashara, ulisaidia

kukuza biashara, ikizingatiwa zaidi kwamba mji huu ulijaliwa kwa asili kuwa na bandari nzuri zaidi

kisiwani. Bandari iligeuka kuwa kituo kikuu cha usambazaji na pia kutoa mwelekeo kamili wa hali ya

biashara katika eneo hili.

Kwa vile mazingira yalikuwa mazuri kwa ajili ya shughuli za kibiashara, watu kutoka mashambani

walihamia mijini, wakisaka nafasi nzuri zaidi za ajira. Kwa misingi hiyo, ardhi ilihitajika kwa kiasi

kikubwa kwa sababu za kibiashara. Zama hizi, Waarabu, Wahindi na Wapersia, walidhibiti umiliki wa

ardhi kiasi cha kulazimisha wenyeji kununua ardhi kutoka kwa wamiliki wake kwa bei kubwa.

Kwa vile wakati huo hapakuwepo mipango mahususi ya kulinda na kudhibiti maendeleo ya makazi

mapya, ilifika hatua watu wakabuni makazi yasiyo na ramani kwenye eneo la Ng’ambo, jambo

lililosababisha makazi kuwa katika hali ya chini, kukosekana huduma za kijamii na miundombinu

muhimu.

Mwaka 1890, Zanzibar iliwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza, Sultani akiwa bado na madaraka

makubwa ya kisiasa hata hivyo. Ni wakati huu ambapo, mipango mbalimbali ilianzishwa na chini ya

mpango huu, Waarabu waliendeleza maeneo ya Kidongo Chekundu, Sebleni, Kwahani na kadhalika.

Kabla ya uhuru, vyama kadhaa vya siasa tayari vilikuwa vikifanya kazi. Vyama vikuu vilikuwa Zanzibar

National Party (ZNP), kilitawaliwa zaidi na wasomi ambao ni wachumi. Chama kingine kilikuwa Afro

Shiraz (ASP), chama kilichokuwa na Waafrika wengi zaidi na kikiwa na mshikamano mkubwa wa

makundi ya wanyonge.

Katika uchaguzi wa mwisho kabla ya uhuru Julai mwaka 1963, ZNP kilichoshirikiana na chama kingine

kidogo cha Pemba, kilifanikiwa kupata wingi wa kura katika baraza jipya la kutunga sheria na Desemba

1963, Zanzibar ilikuwa huru kutoka kwa Waingereza. Mwezi mmoja baadaye, Januari 12 mwaka 1964,

serikali mpya ya Sultani iliangushwa baada ya kufanyika mapinduzi visiwani.

Sultani mwenyewe aliikimbia Zanzibar na ASP ikaingia madarakani na kuitawala nchi hadi mwaka 1977,

kilipoungana na wenzao wa Tanzania Bara, TANU na kuunda Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho

hadi leo kipo madarakani. Licha ya kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar

imekuwa na mamlaka makubwa ya kiserikali kujitawala, isipokuwa kwa masuala ya muungano. Masuala

hayo ya muungano ni kama vile ulinzi, sera za kigeni na mambo ya ndani. Zaidi ya hapo, Zanzibar inalo

Bunge lake, likijulikana zaidi kama Baraza la Wawakilishi lakini pia, inawakilishwa katika Bunge la Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania, ikiwa na wabunge 50 huko.

Mwaka 1995, muswada ulipitishwa na kuwa sheria iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi vya siasa na

katika uchaguzi wa kwanza, CCM ilishinda kama ilivyokuwa tena mwaka 2000 na uchaguzi wa tatu chini

ya mfumo huo utafanyika mwaka 2005.

Manispaa ya Zanzibar iko ndani ya eneo la Mjini Magharibi ambalo limegawanywa katika wilaya kuu

mbili; Wilaya ya Mjini na Wilaya ya Magharibi, kila moja ikiwa na mkuu wa wilaya aliyeteuliwa na rais.

Mipaka ya kiutawala kwa manispaa hii ni kama ile ya Wilaya ya Mjini. Hata hivyo, kwa mujibu wa

michoro iliyotokana na mipango ya mwaka 1982, Mji unachukua eneo kubwa zaidi ya mipaka ya

Manispaa na sehemu yake iko Wilaya ya Magharibi.

Halmashauri ya Manispaa pia, huendesha shughuli zake kwenye maeneo hayo ya Wilaya ya Magharibi,

ambayo kimsingi, yako nje ya mipaka ya awali (lakini ndani ya mipaka iliyowekwa kwa mipango ya Mji).

Mipaka hiyo mipya bado haijaidhinishwa na Wizara ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa kuwa ndiyo

mipaka rasmi ya manispaa.

Hali hii ya utata wa mipaka ya zamani na mipya, inasababisha mgongano kati ya taasisi na vikundi

nyingi. Kwa mfano, madiwani wa Wilaya ya Magharibi, hawapo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya

Zanzibar (ZMC), japokuwa ZMC yenyewe inaendesha shughuli zake. Kwa vile mji umekua na kupanuka

zaidi ya manispaa, inaelekea haitachukua muda, mipaka ya manispaa yenyewe itabadilishwa. Kwa msingi

huo, ripoti hii kwa hiyo, inafuata mipaka mipya iliyopendekezwa na Tume ya Ardhi na Mazingira

(COLE) katika mpango ule wa mwaka 1982

Japokuwa idadi ya kata kwenye Wilaya ya Magharibi ni 10, tatu tu ndizo ziko ndani ya mipaka hii

mipya. Wilaya ya Mjini ina majimbo 13 wakati Wilaya ya Magharibi inazo tatu katika mipaka hiyo mipya.

Kila jimbo huwakilishwa na mbunge na mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye vyombo hivyo vya

kutunga sheria Zanzibar na katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuna jumla ya kata 26 wilayani

Mjini Magharibi na tatu kwenye Wilaya ya Magharibi.

Kata hizo huwakilishwa kwenye Halmashauri ya Manispaa na madiwani wanaochaguliwa. Kwa sasa,

madiwani kutoka Wilaya ya Mjini ndio wanawawakilisha wananchi kwenye Baraza la Manispaa ya

Zanzibar.

Meya huchaguliwa kutoka miongoni mwa madiwani. Kata zimegawanywa tena katika shehia na kila

shehia ina kiongozi anayeitwa sheha. Wilaya ya Mjini ina shehia 39 wakati Wilaya ya Magharibi ina

shehia 23, sita zikiwa ndani ya mipango mipya ya mipaka. Japokuwa bado haijachapishwa kwenye

gazeti la serikali, kuna shehia mpya ya Karakana iliyoko Chumbuni, na hii inafanya jumla ya shehia kuwa

40

Zanzibar, ikijulikana zaidi kama visiwa vya marashi ya karafuu kutokana na sifa ya uzalishaji zao hilo,

inajumuisha visiwa viwili vikubwa ambavyo ni Unguja na Pemba. Manispaa ya Zanzibar iko katikati ya

Pwani ya Magharibi ya Kisiwa cha Unguja. Eneo hili lina ubapa kiasi, huku kukiwa na mwinuko kwa

upande wa magharibi, na kutoka Pwani, kuna mwinuko kidogo, kuelekea mashariki.

Kwa wastani, Pwani yenyewe iko meta 6.6 juu ya usawa wa bahari na eneo lililo lililoko chini zaidi ni

Tomondo, ambako kuna bonde lenye kina cha kati ya meta 10 hadi 15 chini ya usawa wa bahari

Eneo lililo juu zaidi ni tuta la Masingini, meta 100 kwa upande wa mashariki wakati kwa upande wa

magharibi, kuna visiwa vinne ambavyo ni Chapwani, Changuu, Kibandiko na visiwa vya Bawe (tazama

ramani 1.1):

Zanzibar iko kwenye ukanda wa kitropiki na mvua hutegemea kwa kiasi kikubwa majira na mabadiliko

ya pepo za Bahari ya Hindi. Masika ya Zanzibar huzalisha asilimia 40 ya mvua ya mwaka mzima na

huanza Machi hadi Mei. Kipindi cha ukavu, lakini chenye ubaridi kiasi kiitwacho Kusi, huanzia Juni na

kumalizika Septemba wakati Vuli yenye asilimia 20 ya mvua za mwaka mzima, huanzia Oktoba na

kumalizika Desemba. Kipindi cha pepo zitokazo kaskazini kwenda mashariki (Kaskazi), huanza Januari

na kumalizika Machi. mji huu hupata milimita 1,500 hadi 2,000 za mvua kwa mwaka.

Manispaa ya Zanzibar ndio makao makuu ya visiwa hivi na ndio kitovu chake kiuchumi, kisiasa na hata

kitamaduni. Hapa ndio makao makuu ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Huchangia kwa kiasi kikubwa

katika suala zima la biashara na utalii, sekta zinazochangia zaidi mapato ya fedha za kigeni.

Waweza kufika kwenye kisiwa hiki kupitia bandari au uwanja wa ndege wa kimataifa. Ni katika

manispaa hii ya Zanzibar pia, kuna sehemu muhimu kama vile ofisi za Serikali, sehemu za ibada,

biashara na zile za starehe na mapumziko.

Mpangilio wa makazi mjini hapa upo katika aina tano, na umetokana na mipango na taratibu tofauti

zilizoandaliwa (tazama ramani 1.2):

Mji Mkongwe uko upande wa magharibi wa barabara kuu. Ukiwa ndio bandari kongwe, inayotambulika

siku nyingi kihistoria, ina maeneo na majengo yaliyosanifiwa kwa aina yake na ni urithi wa kitamaduni

kwa Wazanzibari na pia ni kivutio kikubwa kabisa cha watalii.

N’gambo ni maeneo mengine makongwe, lakini ambayo hayajachorewa ramani. Yapo upande wa

mashariki wa barabara hiyo na yaliendelezwa kati ya mwaka 1840-1923. Maeneo yenyewe ni

Mwembetanga, Vikokotoni and Kiswandui.

Yapo maeneo mengine ya Ng’ambo yaliyofanyiwa michoro kiasi, kulingana na mipango na taratibu za

mwaka 1958. Maeneo haya ni pamoja na Kidongo Chekundu, Kwahani na Jang’ombe.

Maeneo mapya ambayo bado hayajapimwa, yaliendelezwa mara baada ya kuanzishwa kwa sera za

biashara huria. Haya ni pamoja na Chumbuni, Munduli, Darajabovu, Tomondo, Uholanzi na Kitosani.

Yapo maeneo mapya yaliyopimwa tayari. Maeneo haya yaliendelezwa baada ya michoro iliyoandaliwa

mwaka 1982 na maeneo yenyewe ni Mwanakwerekwe, Mombasa, Mpendae na Chukwani.


mwisho
Usultani Hadi Taifa Huru

Manispaa ya Zanzibar imegawanyika kihistoria katika maeneo mawili, nayo ni Mji Mkongwe na

Ng’ambo. Kuibuka na kukua kwa maeneo haya tangu karne ya 19, kumekuwa katika misingi ya

kiuchumi. Mji Mkongwe uliojengeka vema, ulikuwa kwa ajili ya matajiri na wasomi wakati viunga vya

Ng’ambo, vikawa kwa ajili ya walalahoi.

Mji Mkongwe ulianza kukua taratibu, awali kama makazi ya wavuvi kwenye Rasi ya Shangani katika

karne ya 12. Ulikuwa mji wa Kiswahili hasa, baadhi ya watu wakijishughulisha na sanaa za mikono, na

ikawa sehemu ya biashara zile ndefu zilizofanywa kwa njia ya bahari.

Kunako karne ya 17, Malkia Fatima alipotawala Unguja ya Kati, Mji wa Zanzibar uligeuka na kuwa

makao makuu ya falme yake. Alirithiwa na mwanawe Hasan, anayesemekana alifanya mengi katika

ujenzi wa Mji Mkongwe. Kuingia kwa wafanyabiashara wa Kireno pamoja na wale wa Kiarabu mwaka

1822, kulisababisha Waswahili kuhamia pande za mashariki mwa Mji Mkongwe.

Utawala wa Wareno ulipoanza kusambaratika katika Afrika Mashariki, Waarabu wa Oman, ambao awali

walikuja kama wafanyabiashara, walitwaa madaraka kisiwani Zanzibar. Waligeuza uchumi wa Zanzibar

kutegemea zaidi kilimo cha mashamba makubwa, ndipo uzalishaji wa karafuu ukashamiri na kukipatia

kisiwa umaarufu mkubwa. Japokuwa wamiliki ardhi hiyo walijenga nyumba mashambani, watu wengi

walipendelea zaidi makasri kandokando ya bahari, karibu na hekalu la Sultani.

Eneo ulipokuwa mji wa Zanzibar, lilikuwa jambo la umuhimu mkubwa, hasa wakati Sultani wa Oman,

Seyyid Said alipokuja Zanzibar na akaamua kuufanya kuwa makao makuu. Iliripotiwa kwamba idadi ya

watu kwenye mji huo ilikuwa kati ya 10,000 na 12,000.

Ujio wa Sultani Seyyid Said, ulileta zama mpya kwani mji huo uligeuka kuwa kituo kikuu cha biashara

katika Pwani ya Mashariki mwa Afrika. Misafara ya kibiashara ilistawi kwa kiasi kikubwa na yenye faida

pia, ikihusisha uuzaji watumwa kutoka pwani hii. Watumwa hao walitumiwa kuzalisha bidhaa

mbalimbali pamoja na dhahabu. Biashara ilistawi na misururu kutoka bara, ilileta pembe za ndovu,

dhahabu na watumwa ambao walifanya kazi kwenye mashamba hayo makubwa.

Ni mtawala huyo huyo ambaye aliweka misingi ya kuendeleza mji huu na pia, licha ya karafuu, mazao

mengine yaliyozalishwa kwa kiasi kikubwa ni minazi. Uzalishaji wa mazao haya ya biashara, ulisaidia

kukuza biashara, ikizingatiwa zaidi kwamba mji huu ulijaliwa kwa asili kuwa na bandari nzuri zaidi

kisiwani. Bandari iligeuka kuwa kituo kikuu cha usambazaji na pia kutoa mwelekeo kamili wa hali ya

biashara katika eneo hili.

Kwa vile mazingira yalikuwa mazuri kwa ajili ya shughuli za kibiashara, watu kutoka mashambani

walihamia mijini, wakisaka nafasi nzuri zaidi za ajira. Kwa misingi hiyo, ardhi ilihitajika kwa kiasi

kikubwa kwa sababu za kibiashara. Zama hizi, Waarabu, Wahindi na Wapersia, walidhibiti umiliki wa

ardhi kiasi cha kulazimisha wenyeji kununua ardhi kutoka kwa wamiliki wake kwa bei kubwa.

Kwa vile wakati huo hapakuwepo mipango mahususi ya kulinda na kudhibiti maendeleo ya makazi

mapya, ilifika hatua watu wakabuni makazi yasiyo na ramani kwenye eneo la Ng’ambo, jambo

lililosababisha makazi kuwa katika hali ya chini, kukosekana huduma za kijamii na miundombinu

muhimu.

Mwaka 1890, Zanzibar iliwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza, Sultani akiwa bado na madaraka

makubwa ya kisiasa hata hivyo. Ni wakati huu ambapo, mipango mbalimbali ilianzishwa na chini ya

mpango huu, Waarabu waliendeleza maeneo ya Kidongo Chekundu, Sebleni, Kwahani na kadhalika.

Kabla ya uhuru, vyama kadhaa vya siasa tayari vilikuwa vikifanya kazi. Vyama vikuu vilikuwa Zanzibar

National Party (ZNP), kilitawaliwa zaidi na wasomi ambao ni wachumi. Chama kingine kilikuwa Afro

Shiraz (ASP), chama kilichokuwa na Waafrika wengi zaidi na kikiwa na mshikamano mkubwa wa

makundi ya wanyonge.

Katika uchaguzi wa mwisho kabla ya uhuru Julai mwaka 1963, ZNP kilichoshirikiana na chama kingine

kidogo cha Pemba, kilifanikiwa kupata wingi wa kura katika baraza jipya la kutunga sheria na Desemba

1963, Zanzibar ilikuwa huru kutoka kwa Waingereza. Mwezi mmoja baadaye, Januari 12 mwaka 1964,

serikali mpya ya Sultani iliangushwa baada ya kufanyika mapinduzi visiwani.

Sultani mwenyewe aliikimbia Zanzibar na ASP ikaingia madarakani na kuitawala nchi hadi mwaka 1977,

kilipoungana na wenzao wa Tanzania Bara, TANU na kuunda Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho

hadi leo kipo madarakani. Licha ya kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar

imekuwa na mamlaka makubwa ya kiserikali kujitawala, isipokuwa kwa masuala ya muungano. Masuala

hayo ya muungano ni kama vile ulinzi, sera za kigeni na mambo ya ndani. Zaidi ya hapo, Zanzibar inalo

Bunge lake, likijulikana zaidi kama Baraza la Wawakilishi lakini pia, inawakilishwa katika Bunge la Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania, ikiwa na wabunge 50 huko.

Mwaka 1995, muswada ulipitishwa na kuwa sheria iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi vya siasa na

katika uchaguzi wa kwanza, CCM ilishinda kama ilivyokuwa tena mwaka 2000 na uchaguzi wa tatu chini

ya mfumo huo utafanyika mwaka 2005.

Manispaa ya Zanzibar iko ndani ya eneo la Mjini Magharibi ambalo limegawanywa katika wilaya kuu

mbili; Wilaya ya Mjini na Wilaya ya Magharibi, kila moja ikiwa na mkuu wa wilaya aliyeteuliwa na rais.

Mipaka ya kiutawala kwa manispaa hii ni kama ile ya Wilaya ya Mjini. Hata hivyo, kwa mujibu wa

michoro iliyotokana na mipango ya mwaka 1982, Mji unachukua eneo kubwa zaidi ya mipaka ya

Manispaa na sehemu yake iko Wilaya ya Magharibi.

Halmashauri ya Manispaa pia, huendesha shughuli zake kwenye maeneo hayo ya Wilaya ya Magharibi,

ambayo kimsingi, yako nje ya mipaka ya awali (lakini ndani ya mipaka iliyowekwa kwa mipango ya Mji).

Mipaka hiyo mipya bado haijaidhinishwa na Wizara ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa kuwa ndiyo

mipaka rasmi ya manispaa.

Hali hii ya utata wa mipaka ya zamani na mipya, inasababisha mgongano kati ya taasisi na vikundi

nyingi. Kwa mfano, madiwani wa Wilaya ya Magharibi, hawapo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya

Zanzibar (ZMC), japokuwa ZMC yenyewe inaendesha shughuli zake. Kwa vile mji umekua na kupanuka

zaidi ya manispaa, inaelekea haitachukua muda, mipaka ya manispaa yenyewe itabadilishwa. Kwa msingi

huo, ripoti hii kwa hiyo, inafuata mipaka mipya iliyopendekezwa na Tume ya Ardhi na Mazingira

(COLE) katika mpango ule wa mwaka 1982

Japokuwa idadi ya kata kwenye Wilaya ya Magharibi ni 10, tatu tu ndizo ziko ndani ya mipaka hii

mipya. Wilaya ya Mjini ina majimbo 13 wakati Wilaya ya Magharibi inazo tatu katika mipaka hiyo mipya.

Kila jimbo huwakilishwa na mbunge na mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye vyombo hivyo vya

kutunga sheria Zanzibar na katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuna jumla ya kata 26 wilayani

Mjini Magharibi na tatu kwenye Wilaya ya Magharibi.

Kata hizo huwakilishwa kwenye Halmashauri ya Manispaa na madiwani wanaochaguliwa. Kwa sasa,

madiwani kutoka Wilaya ya Mjini ndio wanawawakilisha wananchi kwenye Baraza la Manispaa ya

Zanzibar.

Meya huchaguliwa kutoka miongoni mwa madiwani. Kata zimegawanywa tena katika shehia na kila

shehia ina kiongozi anayeitwa sheha. Wilaya ya Mjini ina shehia 39 wakati Wilaya ya Magharibi ina

shehia 23, sita zikiwa ndani ya mipango mipya ya mipaka. Japokuwa bado haijachapishwa kwenye

gazeti la serikali, kuna shehia mpya ya Karakana iliyoko Chumbuni, na hii inafanya jumla ya shehia kuwa

40

Zanzibar, ikijulikana zaidi kama visiwa vya marashi ya karafuu kutokana na sifa ya uzalishaji zao hilo,

inajumuisha visiwa viwili vikubwa ambavyo ni Unguja na Pemba. Manispaa ya Zanzibar iko katikati ya

Pwani ya Magharibi ya Kisiwa cha Unguja. Eneo hili lina ubapa kiasi, huku kukiwa na mwinuko kwa

upande wa magharibi, na kutoka Pwani, kuna mwinuko kidogo, kuelekea mashariki.

Kwa wastani, Pwani yenyewe iko meta 6.6 juu ya usawa wa bahari na eneo lililo lililoko chini zaidi ni

Tomondo, ambako kuna bonde lenye kina cha kati ya meta 10 hadi 15 chini ya usawa wa bahari

Eneo lililo juu zaidi ni tuta la Masingini, meta 100 kwa upande wa mashariki wakati kwa upande wa

magharibi, kuna visiwa vinne ambavyo ni Chapwani, Changuu, Kibandiko na visiwa vya Bawe (tazama

ramani 1.1):

Zanzibar iko kwenye ukanda wa kitropiki na mvua hutegemea kwa kiasi kikubwa majira na mabadiliko

ya pepo za Bahari ya Hindi. Masika ya Zanzibar huzalisha asilimia 40 ya mvua ya mwaka mzima na

huanza Machi hadi Mei. Kipindi cha ukavu, lakini chenye ubaridi kiasi kiitwacho Kusi, huanzia Juni na

kumalizika Septemba wakati Vuli yenye asilimia 20 ya mvua za mwaka mzima, huanzia Oktoba na

kumalizika Desemba. Kipindi cha pepo zitokazo kaskazini kwenda mashariki (Kaskazi), huanza Januari

na kumalizika Machi. mji huu hupata milimita 1,500 hadi 2,000 za mvua kwa mwaka.

Manispaa ya Zanzibar ndio makao makuu ya visiwa hivi na ndio kitovu chake kiuchumi, kisiasa na hata

kitamaduni. Hapa ndio makao makuu ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Huchangia kwa kiasi kikubwa

katika suala zima la biashara na utalii, sekta zinazochangia zaidi mapato ya fedha za kigeni.

Waweza kufika kwenye kisiwa hiki kupitia bandari au uwanja wa ndege wa kimataifa. Ni katika

manispaa hii ya Zanzibar pia, kuna sehemu muhimu kama vile ofisi za Serikali, sehemu za ibada,

biashara na zile za starehe na mapumziko.

Mpangilio wa makazi mjini hapa upo katika aina tano, na umetokana na mipango na taratibu tofauti

zilizoandaliwa (tazama ramani 1.2):

Mji Mkongwe uko upande wa magharibi wa barabara kuu. Ukiwa ndio bandari kongwe, inayotambulika

siku nyingi kihistoria, ina maeneo na majengo yaliyosanifiwa kwa aina yake na ni urithi wa kitamaduni

kwa Wazanzibari na pia ni kivutio kikubwa kabisa cha watalii.

N’gambo ni maeneo mengine makongwe, lakini ambayo hayajachorewa ramani. Yapo upande wa

mashariki wa barabara hiyo na yaliendelezwa kati ya mwaka 1840-1923. Maeneo yenyewe ni

Mwembetanga, Vikokotoni and Kiswandui.

Yapo maeneo mengine ya Ng’ambo yaliyofanyiwa michoro kiasi, kulingana na mipango na taratibu za

mwaka 1958. Maeneo haya ni pamoja na Kidongo Chekundu, Kwahani na Jang’ombe.

Maeneo mapya ambayo bado hayajapimwa, yaliendelezwa mara baada ya kuanzishwa kwa sera za

biashara huria. Haya ni pamoja na Chumbuni, Munduli, Darajabovu, Tomondo, Uholanzi na Kitosani.

Yapo maeneo mapya yaliyopimwa tayari. Maeneo haya yaliendelezwa baada ya michoro iliyoandaliwa

mwaka 1982 na maeneo yenyewe ni Mwanakwerekwe, Mombasa, Mpendae na Chukwani.


mwisho

Sunday, March 18, 2007

kwanini wanaume hufika kileleni mapema?

Na Aisha Mbaga

Kwanini wanaume hufika kileleni mapema

Hiyo ni kutokana na kushindwa kujidhibiti wakati wa mechi hadi pale wote wawili mtakapokuwa mtakaribia kufunga goli muweze kufunga pamoja.

Kufika kileleni mapema ni tatizo linalowakabili wanaume wengi wakati wa mapenzi. Mara nyingi tatizo hili hutokea katika siku ya kwanza kabisa mwanaume akutanapo na mwanamke ampendaye au anayeanzisha uhusiano nae kwa mara ya kwnza kukutana ni jambo la kawaida kwa mwanaume kushindwa kujimudu na kujikuta kafunga goli wakati mwenzake ndo kwanza anawasha moto.

Mwanaume anapomsotea mwanamke kwa muda mrefu, siku akimpata basi ni lazima mwanaume huyo kujikuta anashindwa kuucheza mchezo kiufundi na kujikuta kapanda mnazi na kuzdondosha zake kabala mwenzi wake hajafika popote.

Hata hivyo kua katika hali hii si ugonjwa bali ni hali ya kawaida tu ingawaje humfanya mmoja wenu kutofurahia na kujikuta akiwa na hamu ya kuendelea huku mwingine kachoka.pia kibaiolojia, tatizo hili linasababishwa na ukosefu wa uwiano wa “Homon” ikiwa homona zenu hazija zoeana, mwanaume anaweza kuona kuwa mwanamke hana ladha ile anayoitaka.

Sababu hiyo inaweza kumsababisha mwanaume kuvuta hisia kwa kumkimbuka mwanamke ambaye humfikisha na kumpa ladha anayoitaka ili aweze kukamilisha tendon a mwanake aliyenaye ka wakati huo hivyo anaweza akajikuta akilitaja jina la mwanamke mwingine wakati yuko na mwanamke mwingine.

Kisaikolojia hali ya kufika kileleni mapema bila mpangilio inasababisha na kushindwa kujiamini kwa mwanaume. Hapa ni kwa yule mwanaume aliyemsotea mwanamke kiasi cha kufikia hatua ya kukaribia kukata tama na baadae kujikuta kafanikiwa.

Mwanaume huyo huwa na kimuhemuhe cha kumpanda mwanamke huyo hivyo kujikuta kuwa amuonapo tu mrembo wake yeye anakuwa hahitaji tena maandalizi na ukimchekeweshea anaharibu mambo kabla ya kuanza kulili tunda lenyewe.

Kutokana na kutojiamini kwake, mwanuame huyo atakuwa akiwaza kama ni kweli ama ni ndoto kuwa na kimwana kama huyo aliye masotea kwa muda mrefuna sasa amefanikiwa kumuweka katika mikono yake, lazima mwanaume huyu atachetuka avuliwapo nguo na mwanadada huyu.

Kwa kawaida wanaume wengi hupenda wafanye mapenzi kwa dakika nyingi zaidi ili mwawa firahishe wapenzi wao lakini bila ya kutarajia wanajikuta wakiwa wamezidiwa nguvu na vimwana wao na hiyo ni kutokana na kuwa haijalishi kuwa ni muda gani maalumu wa mwanaume anatakiwa awe anafanya mapenzi kabla ya kufika kileleni.

Hebu tujiulize kwamba kuna ambaye anaweza kujizuia kufika kileleni mapema? Jibu ni kwamba unaweza ila cha msingi ni kuwa mtulivu na kuondfokana na wasiwasi, yaani unapaswa kujiamini kuwa unawza na umeshinda kuwa na huyo.

Usifanye mapenzi kwa kukomoa na wala usipanie sana kuwa lazima nikikutana na e niingie, jiamini kuwa ni wako na muda wote uko naye na unaweza kuchezanae upendavyo kwa kutumia muda wako.

Nimuhimu kujitambua kuwa utafika kileleni kwa wakati gani hivyo unaweza kujizuiakatika hatua hii muhimu kwa kujifunza na kuzoea.

Basi mpenzi msomaji wa safu hii napenda kukuaga kwa leo ila nakusihi tujumuike soto katika safu hii toleo lijalo. Kwa maswali au maoni wasiliana nami kwa barua pepe: aishamudysaan@yahoo.com au simu namba 0755-690690.

Mwisho.

Kwanini wanaume husaliti penzi

kwanini wanaume husaliti penzi?

Na Aisha Mbaga

Mpenzi Msomaji wa safu hii, nakukaribisha tena tujumuike katika
Chumba cha Mahaba n ipate kukupa dondoo mbali mbvali juu ya
kuimarisha mepenzi na kujitambua zaidi juu ya swala zima la
mahaba.

Wiki iliyopita tulizungumzia juu ya matayarisho ya chumba cha
mahaba nikijumuisha na mbambo muhimu wakati wa
kujimwayamwaya na mpenzio, pia tulizungumzia juu ya matayarisho ya kitanda na jinsi ya usafi umalizapo mechi yako.

Leo mpenzi msomaja wa Tanzania Daima ndani ya Chumba cha
Mahaba tunazungumzia ni kwanini wanaume wengi hupenda kutoka nje ya ndoa zao ama kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja.

Haimananishi kuwa mwanaume anapotoka nje ya mwenzi wake
amemchoka ama hamtaki, kinachotokea ni kwamba mwanaume
huvutwa na hali halisi ya maumbile ya mwanamke na kila wakati
hupenda kutafuta ladha fulani.

Kujua kuwa mwanaume huyo anamheshimu mpenzi wake wa
kudumu, atakuwa anafanya mapenzi hayo ya wizi kwa siri ili mpenzi wake ama mkewe asitambuwe kuwe anaibiwa.

Maranyingi wanawake huwa hawapendi kuwaona wenzi wao wakiwa na uhusiano wa mapenzi na mwanamke mwingine zaidi yake hivyo huwa na wivu mkubwa juu ya mpenziwake kufikia hatua ya kuwekeana uhasama na mwanamke atakayemgundua kuwa anamwibia penzi lake.

Ugomvi mwingi wa wanawake unakuja pale ambapo wanajikuta
wakishea mwanaume mmoja na kwa wkati mmoja huku kila mmoja akiwa na tumaini kuwa yuko pekeyake na mwanaume huyo kumtimizia kila mmoja haki yake kwa muda wake.

wanawake hao watakapogunguana, ajabu wanawekeana uhasama wao kwa wao bila kujua kuwa kati yao hakuna mwenye kosa kwani kila mmoja kwatakwa kwa muda wake na wakumlaumu ni yule mwanaume ndiye wangepaswa kukkaba awaeleze kinagaubaga.


Haimaanishi kwamba wanume ni malaya sana kuliko wanawake ndio maana hawatosheki matamanio yao, lahasha! hapa tunayazungumzia maumbile ya mwanaume kutokana
na kuvutika kihisia kwa mwanamke yeyote amwonaye kuwa na mvuto kwake.

Wakati mwingine wanawake tumekuwa kivutio kwa wanaume na
kuwaweka katika wakati mgumu huku tukielewa wazi kuwa
tunawatega. pamoja na kuwa tunakwenda na wakati, tunapaswa
kujua kuwa mwanamke hata avae juba, mwanaume akishamtamani lazima akidhi haja ya matamanio yake hata kama hatafanikiwa kwa mwanamke huyo, basi atatafuta mwanamke anayeendana na huyo.

hayo ndiyo maumbile ya mwanaume hivyo kwa mwanamke mwenye wivu unaweza ukajidhani labda humvutii mpenzi wako ama hupendezu kumbe wewe ni mzuri na unawavutia wanaume wengi kwani hakuna mwanake asiyekuwa na mvuto mbele ya mwanaume.

Ili kujua kuwa mwanaume anakupenda ila hufanya kosa kutokana
na maumbile yake, ni pale utakapomfumania akikusaliti, mwingine hukosa raha ama akajikuta akilia kujutia alichokifanya huku akiwa na hofu ya kuachwa.

Mwanaume mwingine huwa anakosa cha kuongea na
kupata kigugumizi cha ghafla ama kujikuta akikudanganya juu ya tukio hilo kuwa hakutegemea kama ingetokea, “Hakkujua kama angefanya”
kwa wanaume wengine hukujia juu ili kukupunguza jazba ama kukutisha ili usimuulize chochote na kisha baadae hukuomba msamaha. hizi zote ni baadhi ya tabia na maumbile ya wanaume.

Wapo ambao wanawatetea wanawake wanaofumaniwa nao kwa ajili ya kuwalinda isi wasidhuriwe na mwanamke muhusika kwani yawezekana lolote likatokea kati yao kisha mwanaume yule akaja kukuomba radhi na kukusihi kuwa hatorudia kosa hiyo imetokea kwa bahati mbaya akashindwa kujizuia.
Jinsi ya kujikinga na na kujaribu kumfanya mpenzi wako asiwe na
tamaa, mwache awe huru na mjengee mazingira ya kuona wivu na
kuhisi kuwa anaibiwa. kwa kufanya hiyo unaweza ukamweka
mwanaume wako katika mtihani na kumpa kazi kubwa ya
kukufuatilia hatua hadi hatua na kujikuta akikosa muda wa
kuwatizama wanawake wengine hivyo unakuwa umemwondolea tabia ya kuwatamani wanawake ovyo na kumpa kazi ya kukuchunga.

Haimaanishi kuwa mkawafanyae waume zenu hivyo, kwa kuwakomoa, jaribuni kuwafanyia ili kutengeneza penzi lenu. wapo ambao hawajali ukimwacha huru anashukuru na anakuwa naye anakuacha huru japo atakuwa anaumia kuwa huenda anaibiwa, atauficha wivu wake juu yako.

Hakuna mwanaume anayependa kuona kuwa anashea mwanamke na mwanaume mwenzake, huwa inawaweka katika wakati mgumu na niadhabu kubwa inayowaumiza japo wanakuwa jasiri tofauti na wanawake wanaoishia kulia na kujikondesha.

Hii ni tabia ya baadhi ya wanaume wengi kwani wivu wao upo
ndani na unawaumiza ndani kwa ndani lakini hawapendi
kuwaonyesha wanawake kuwa wanawivu juu yao.

mwanaume huwa atakuuliza tu kuwa yule ni nani na kwanini umesimama naye ama umekaa naye sehemu ya stare au faragha kama hiyo na hapo hapo atataka mchezo ili kuhakikisha kuwa hakuna aliyepita kwenye njia yake.

Nataka nikwambie jambo moja wewe mwanake mwenzangu ambaye unadhani kuwa labda mpenzio anakuona humzuri ndio maana anatoka nje na kukuacha ndani pekeyako.

kwanza usisuburikusifiwa kuwa wewe ni mzuri, cheo hicho jipe mwenyewe na anayekuona kuwa wewe ni mbaya usimkataze kufikiri hovyo kwani huo ni matazamo wa akili yake unavyodhani lakini amini wewe umzuri kuliko mtu mwingine yeyeto.

Pia usipende kumsema mwanamke mwenzio kuwa si mzuri, Mungu hajaumba binadamu mvbaya ila tabia ndio zinatofautiana kutokana na maumbile ya nafsi ya mtu mwenyewe upeo wa akili zetu.

Mwanaume wako anapotoka nje na ukajua, usimwambie chochote
zaidi ya kumsifia kuwa anachombo kipaya na kizuri kisha mpe
hongera na atakapo mambo fulani mpe, utakapomfanyia hivyo
utamnyima raha kwa kujutia alichokifanya na kuwaza kwanini
amekusaliti.

Japo kuwa ni maumbikle yamempelekea kufanya hivyo, atajilaumu na wakati mwingine atakuwa anataka kukufanyia jambio ili usahau ama umsamehe zaidi kosa lake la kusaliti penzi.
wakati mwingine wanawake wanapowafumania waume zao huanza kuropoka na kuwatukana, mmm! hatuendi hivyo dada yangu,
unapomfumania mwanaume wako msifie kwa urijali wake na kisha nyamaza kimya bila kumuuliza chochote.
kama ilivyo kawaida ukimya ni adhabu kwa wapendanao, unaponyamaza atataka kujua kuwa unafikiria nini kichwani kwako, atakosa raha kwa kujua kuwa huenda ukalipiza kisasi, atawaza
mengi juu ya ukimya wako na ukamfanyia hivyo kwa wiki moja, ukaenda kumpima uzito atakuwa amepungua.
yapo mambo mengine yanayopelekea mwanaume kusaliti penzi lake
kutokana na jinsi mpenzi wake anavyojiweka tofauti na kuwa maumbile ya mwanaume ni yamatamanio aonapo maumbile ya mwanamke.

Uchafu wa mwanamke nao unasababisha mwanaume kukimbilia anapoona kuwa panausafi na pengine kujikita huko kabisa japo wanadai kuwa gari huwa lazima ipate spea tairi, waweza ukajikuta
kuwa, mazingira uliyonayo yanakufanya wewe ndiye spea kuliko spea yenyewe.

Nataka kuwashauri wanawake wenzangu kuwa mwanamke mazingira.
Kujipakaa mafuta usoni ukang'aa lakini kule Ikulu iliyokufanya wewe ukaitwa binti na kuonekana mrembo huifanyii usafi kiasi cha kumkera kila anayeingia, jua utakuwa mtanashati wa uso na mavazi tu lakini kwimgineko mh! Hapafai.

Tambua kuwa hiyo Ikulu yako ndiyo inawasababisha hao wanaume mpaka wanapigana, yote ni kwasababu tu inamvuto na ndio maana waweza kumuona mwanaume anamng’ang’ania mwanamke ambaye hawaendani, eidha mwanaume ni mzuri sana kuliko mwanamke lakini hiyo si tija cha msingi ni umaridadi wa Ikuli.

Wahenga walisema si vyote ving'aavyo ni dhahabu ati, pia Uzuri wa mkakasi ndani kipande chamti na mimi nakwambia kuwa, kaa na marashi nawe unukie japo hujajipulizia lakini ukaapo na wenye
marashi nawe waweza onekana ni miongoni wao kumbe la.

Napenda wanawake tupunguze wivu na kwani unasababisha kujengeana majungi na wakati mwingine kudhiriana hata kwa kuuwana kisa ni wanaume ambao hata ufanye nini hakuna mwanaume wa pekeyako. Kasema hadija kopa kuwa Kamaunaweza
mtie kamba mumeo lakini ukitahamaki kachimba chini ninaye.

Basi mpenzi msomaji wa safu hii nisikumalizie uhondo kwa siku ya leo, nakushukuru kwa
kuungana nami. basi mpenzi msomaji tukutane wiki ijayo katika chumba hiki hiki cha mahaba na tutakuwa tunazungumzia ni kwanini wanaume huwahi kumaliza tendo la ndoa kabla ya wanawake.

Kwa ushauri au maoni wasiliana nami simu ya kiganjani namba 0755-690690 au
nitumie ujumbe kupitia baruapepe yangu aishamudysaan@yahoo.com.

Friday, March 16, 2007

mapenzi ni nguzo ya kujenga familia

Na Aisha Mbaga

Mengi yameongelewa na yatazidi kuongelewa kuhusiana na hali halisi katika uwanja wa mapenzi.

Mimi nazungumzia hali hiyo lakini katika upande wa kuanzisha , kuboresha na kuyalinda mapenzi ya dhati.

Nimekusudia kukutandikia uwamja huu kwa sababu mapenzi ni kitu kisichokwepeka.

Hakuna binadamu anayeweza kukyakwepa mapenzi, kukwepa kupenda ama kupendwa kutokana na kuwa hayo ni maumbile.

Kwa kawaida mtu umpendae kuwa hukosi hamu ya kuonana naye kama ilivyo kwa mama na mwana ama mwana na mama ila katika mapenzi ya msichana na mvulana mambo hubadilika na kuwa ya ndani zaid.

Ukiwa na hamu ha hali ya juu kwa mpenzio basi upo katika kilele cha mapenzi na hutakiwi kushuka kwani ukiona unashuka kiwango cha kumuona mpenzio basi ujue kunahatari ya kusambaratika kwa mapenzu yenu.

Napenda kuanzia kukiandaa chumba cha mapenzi, ama uwanja wa mapenzi. Si lazima iwe kitandani tu, waweza badili uwanja kwa kuhamia bafuni ama kochini nap engine gaeini.

Kwanza kisafishe chumba chako vizuri kwa kifita vumbi kila kona .

Hakikisha kuwa unakipamba chumba chako kwa mauwa na kadi kama unazo.

Kifukize chumba chako udi ili kukifanya kinykie vizuri ama kipulizie marashi ya sluud kama unauwezo nayo, kama huna waweza tumia hata air freshna.

Kinachotakiwa ni kuiandaa sehemu yenyewe. Kama kitandani, tandika kitanda chako vizuri kwa shuka lemuye mauwa ya kuvutia, kama ni jeupe na halina mauwa, waweza kuchukua mauwa ya asumini ukayamwaga kitandani bna kuyatandaza vizuri. Ukikosa asumini waweza tumia mauwa ridi,. Mauwa haya huwa yanaharufu nzuri.

Waweza yatandaza nyumba nzima kama waweza ama chumba kizima kiwe kinanukia asumini,

Baada ya hapo hakikisha kuwa unausafisha mwili wako vizuri na kuuweka safi kwa ajili ya kuingia uwanjani kucheza mechi ya mahaba.

Fahamu kuwa kunamaks ambazo unaweza kuzipata ukiwa uwanjani ama ukazikosa hivyo ili kujiweka katika kiwango cha juu cha ufundi wa kufunga magoli ya mapenzi, ni lazima uwe na juhudi, usichoke na uwe makini katika mchezo ili uhakikishe mnatoka sare kwa kufunga goli.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umefaulu mechi yako na utajiweka katika nafasi ya juu kiasi cha kumfanya mpenzio kukukumbuka kila awapo.

Sasa nakupeleka katika kuuandaa mwili wako.

Nenda bafuni uoge vizuri na ujisafishe sehemu zako zote nyeti za mili vizuri kwa kuuweka mili wako safi ili mpenzio aweze kuutembelea apendavyo.

Jitie manukato laini. Jifukize ikili yako udi na hakikisha kuwa wakati wa kujifukiza unamimina marashi ya aluud ili kuiruhusu harufu nzuri kupenya sehemu zote.

Fukiza nyele zako na nguo zako utakazovaa kabla ya kuingia uwanjani.

Andaa kitezo chako na moto kisha kiweke udi na uendelee kupendezesha chumba chako.

Andaa kitambaa cha pamba, mji ya mojo kwenye chupa na kibeseni kwa ajili ya kujisafisha mara baada ya mechi wewe na mpenzio.

Aingiapo mpenzio tia marashi ya aluud kwenye kitezo kisha mkaribishe uwanjani na muanze na mazoezi kabla ya mechi kali.

Wakati mnaendelea na mechi udi na marashi ya aluud yanapenya kwenye miili yenu taratibu na kuburudisha.

Kumbuka kutumia kitambaa chako laini kujisafishia taka zote baada ya mechi kali kisha nendeni wote bafuni mkaoge. Ikiwezekana endeleeni kujipa raha humohumo bafuni.

Ka leo tuishie hapo ila nakusihi usikose kujiunga nami toleo lijalo. Kwa maoni ushauri, wasiliana nami kwa barua pepe. aishamudysaan@yahoo.com au simu ya kiganjani 0755690690.
mapenzi ni nguzo ya kujenga familia

Na Aisha Mbaga

Mengi yameongelewa na yatazidi kuongelewa kuhusiana na hali halisi katika uwanja wa mapenzi.

Mimi nazungumzia hali hiyo lakini katika upande wa kuanzisha , kuboresha na kuyalinda mapenzi ya dhati.

Nimekusudia kukutandikia uwamja huu kwa sababu mapenzi ni kitu kisichokwepeka.

Hakuna binadamu anayeweza kukyakwepa mapenzi, kukwepa kupenda ama kupendwa kutokana na kuwa hayo ni maumbile.

Kwa kawaida mtu umpendae kuwa hukosi hamu ya kuonana naye kama ilivyo kwa mama na mwana ama mwana na mama ila katika mapenzi ya msichana na mvulana mambo hubadilika na kuwa ya ndani zaid.

Ukiwa na hamu ha hali ya juu kwa mpenzio basi upo katika kilele cha mapenzi na hutakiwi kushuka kwani ukiona unashuka kiwango cha kumuona mpenzio basi ujue kunahatari ya kusambaratika kwa mapenzu yenu.

Napenda kuanzia kukiandaa chumba cha mapenzi, ama uwanja wa mapenzi. Si lazima iwe kitandani tu, waweza badili uwanja kwa kuhamia bafuni ama kochini nap engine gaeini.

Kwanza kisafishe chumba chako vizuri kwa kifita vumbi kila kona .

Hakikisha kuwa unakipamba chumba chako kwa mauwa na kadi kama unazo.

Kifukize chumba chako udi ili kukifanya kinykie vizuri ama kipulizie marashi ya sluud kama unauwezo nayo, kama huna waweza tumia hata air freshna.

Kinachotakiwa ni kuiandaa sehemu yenyewe. Kama kitandani, tandika kitanda chako vizuri kwa shuka lemuye mauwa ya kuvutia, kama ni jeupe na halina mauwa, waweza kuchukua mauwa ya asumini ukayamwaga kitandani bna kuyatandaza vizuri. Ukikosa asumini waweza tumia mauwa ridi,. Mauwa haya huwa yanaharufu nzuri.

Waweza yatandaza nyumba nzima kama waweza ama chumba kizima kiwe kinanukia asumini,

Baada ya hapo hakikisha kuwa unausafisha mwili wako vizuri na kuuweka safi kwa ajili ya kuingia uwanjani kucheza mechi ya mahaba.

Fahamu kuwa kunamaks ambazo unaweza kuzipata ukiwa uwanjani ama ukazikosa hivyo ili kujiweka katika kiwango cha juu cha ufundi wa kufunga magoli ya mapenzi, ni lazima uwe na juhudi, usichoke na uwe makini katika mchezo ili uhakikishe mnatoka sare kwa kufunga goli.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umefaulu mechi yako na utajiweka katika nafasi ya juu kiasi cha kumfanya mpenzio kukukumbuka kila awapo.

Sasa nakupeleka katika kuuandaa mwili wako.

Nenda bafuni uoge vizuri na ujisafishe sehemu zako zote nyeti za mili vizuri kwa kuuweka mili wako safi ili mpenzio aweze kuutembelea apendavyo.

Jitie manukato laini. Jifukize ikili yako udi na hakikisha kuwa wakati wa kujifukiza unamimina marashi ya aluud ili kuiruhusu harufu nzuri kupenya sehemu zote.

Fukiza nyele zako na nguo zako utakazovaa kabla ya kuingia uwanjani.

Andaa kitezo chako na moto kisha kiweke udi na uendelee kupendezesha chumba chako.

Andaa kitambaa cha pamba, mji ya mojo kwenye chupa na kibeseni kwa ajili ya kujisafisha mara baada ya mechi wewe na mpenzio.

Aingiapo mpenzio tia marashi ya aluud kwenye kitezo kisha mkaribishe uwanjani na muanze na mazoezi kabla ya mechi kali.

Wakati mnaendelea na mechi udi na marashi ya aluud yanapenya kwenye miili yenu taratibu na kuburudisha.

Kumbuka kutumia kitambaa chako laini kujisafishia taka zote baada ya mechi kali kisha nendeni wote bafuni mkaoge. Ikiwezekana endeleeni kujipa raha humohumo bafuni.

Ka leo tuishie hapo ila nakusihi usikose kujiunga nami toleo lijalo. Kwa maoni ushauri, wasiliana nami kwa barua pepe. aishamudysaan@yahoo.com au simu ya kiganjani 0755690690.
UHUMI WA TANZANIA UTABOREKA TU



Na Aisha Mbaga
RAIS wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania, Jakaya Kikwete, amesema serikali ya awamu ya nne itaendelea kuamini kuwa, sekta binafsi ni moyo wa uchumi na maendeleo ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.
Kikwete alisema kuwa, Serikali, imeweka mazingira mazuri katika kuhakikisha kuwa, fursa zote zilizopo kwenye uwekezaji, zinatumika kikamilifu kwa manufaa ya Taifa.
Hali kadhalika, alieleza kwamba, amewataka wawekezaji wa nje na ndani, kujenga imani na serikali yake ambayo alisema itafanya kazi na wadau hao kwa faida ya pande zote.
Katika Mkutano wa sita ulioandaliwa na Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) uliofanyika mjini arusha, aliwataka wawekezaji kuwa na imani na Tanzania kwani ni nchi ambayo inaamani na inayopiga hatua kimaendeleo.
Lengo la mkutano huo ilikuwa n i kujadili masuala muhimu ya kiuchumi yatakayoiwezesha Tanzania kuondokana na mfumo wa uchumi hodhi.
Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa TNBC, alisema kwa kuthamini mchango unaotolewa na wawekezaji wa ndani na nje, serikali yake imekuwa ikifanya mabadiliko katika baadhi ya sheria za biashara, zilizoonekana kukwamisha mikakati ya kuwezesha wawekezaji wa nje kuja nchini kuwekeza, hususan wa sekta za viwanda, madini na kilimo.
Alitaja baadhi ya sheria ambazo zimekuwa changamoto kwa wawekezaji wa ndani na nje zilizofanyiwa marekebisho kuwa ni ya ardhi na sheria ya kazi ambayo wawekezaji wengi ama waajiri wengi, wamekuwa wakidai kwamba, zinawakandamiza mno waajiri na kuwapendelea zaidi waajiriwa.
Alisema Kikwete Kuwa, "Kwa kuthamini mchango wa wawekezaji ambao wamekuwa wakisaidia maendeleo ya taifa, hususani katika suala la mapato ya serikali kutokana na biashara wanazoziendesha, serikali imekuwa ikijiendesha kutokana na kodi zinazotozwa toka kwenye sekta binafsi",.
Alisema, tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeaanza kuangalia sheria hizo.
Alitaja hatua nyingine ambayo serikali ipo kwenye mchakato wa kuifanyia marekebisho kuwa ni ya vibali na leseni za biashara hapa nchini, hususan kwa wawekezaji wa nje.
Alisema kupitia mkutano uliopita wa Baraza la Taifa la Wafanyabiashara, wawekezaji wa nje walieleza kwamba changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni vibali vya kufanyia biashara kuwa vya bei ghali ikiwa ni pamoja na urasimu wa kuvipata.
Rais Kikwete alisema, tayari ameziagiza mamlaka husika, kuangalia upya suala hilo ambapo alieleza kwamba, kiwango cha kulipia vibali vya kufanya biashara hapa nchini kitapunguzwa kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Aidha alisema, "azma ya serikali kwa kushirikiana na baraza hilo ni kuhakikisha sekta binafsi zinapewa nafasi ya kuongoza ujenzi wa uchumi wa nchi, huku serikali ikiwa na kazi moja ya kujenga mazingira bora zaidi ya ufanyaji biashara".
"Natumaini kupitia mkutano huu, kasi dhidi ya ukuaji wa uchumi wa Taifa letu itaongezeka maradufu kupitia sekta binafsi zitakazowekeza hapa nchini, hasa kwa upande wa elimu, kilimo, utalii, viwanda, miundombinu, mawasiliano na sekta ya madini", alisema Rais Kikwete.
Hata hivyo, aliwataka wawekezaji kushirikiana na serikali katika kuboresha miundombinu, hususan ya barabara, ambapo alisema wawekezaji nao ni muhimu wakachangia ujenzi wa barabara badala ya suala hilo kuachiwa serikali pekee.
Kutokana na mabadiliko ya utandawazi pamoja na kuongezeka kwa gharama za kuendeshea sekta ya utalii, Rais alisema kuwa serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ipo kwenye mpango wa kuongeza kodi ya watalii wanaoingia nchini kila mwaka kwa ajili ya kutembelea mbuga za wanyama.
Alisema gharama zimekuwa ni ghali mno kuliko awali hasa suala la kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ya hifadhi za Taifa pamoja na barabara zinazokwenda kwenye hifadhi hizo.
"Serikali iko kwenye mchakato wa kuongeza kodi za watalii wanaoingia, ili kuboresha huduma ya utalii na kuongeza pato la Taifa", alisema JK.
Kuhusu suala la sekta ya kilimo, Rais Kikwete alisema kwa kuthamini kilimo ambacho ndicho uti wa mgongo wa taifa, kwa sasa serikali inaandaa mpango ya kuboresha sekta hiyo kwa njia ya kilimo cha umwagiliaji na utumiaji wa mbolea ili kuleta tija zaidi.
"Katika sekta ya kilimo, bado tunazidi kujitangaza ili kuzidi kuwavutia wawezekaji, kwani sekta hii ndio kitega uchumi cha Watanzania wengi na tegemeo kubwa kwa taifa letu", alisema Kikwete.
Alisema, kwa sasa kilimo cha umwagiliaji ndicho kinachopewa kipaumbele, ambapo aliwataka wawekezaji wa sekta ya kilimo kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza hasa ikizingatiwa kwamba Tanzania ina vyanzo vingi vya maji kama mabwawa, mito, mifereji ambayo inafaa kwa kilimo cha umwagiliaji.
mwisho.
WANANCHI NA UCHUMI WA tANZANIA


Mara nyingi hotuba za viongozi wakuu wa serikali za awamu ya tatu na ya nne wamekuwa wakizungumzia juu ya kuimarika kwa uchumi baada ya marekebisho mbalimbali ya sera za uchumi. Benki Kuu ya Tanzania huwa inazungumzia mambo ya mfumuko ya bei, viwango vya ubadilishaji wa fedha za kigeni na riba za mabenki na taasisi za fedha ili kuelewa tumetoka wapi katika safari ya kuimarisha uchumi. Ni muhimu kuangalia hali ya uchumi wa miaka kumi na tano iliyopita katika miaka ya mwazo ya miaka ya 1990. Kati ya mwaka 1990 hadi 1995 mfumuko wa bei yaani ongezeko la bidhaa zote za mlaji zilikuwa zinaaongezeka kwa kati ya asilimia 30 hadi asilimia 36 kila mwaka. Kwa hali hiyo fedha ilipoteza thamani kwa sababu uwezo wake wa kununua bidhaa ulipunguka sana. Wakati huo vile vile ilibidi riba zinazotozwa na kutolewa na mabenki kwa amana ilibidi ziongezeke kwa sababu ya kuteremka kwa bei. Benki ingepata hasara kama ingekopesha fedha kwa riba ya asilimia kumi wakati mfumuko wa bei ulikuwa asilimia thelathini vile vile wakaweka fedha zao katika mabenki ilibidi walipwe riba za amana za juu ingawa hii haikuwezekana kwa sababu benki zilikuwa mbili NBC na CRDB zilikuwa na ukiritimba wa shughuli za benki na wawekezaji amana hawakuwa na uchaguzi wa wapi waweke amana zao ili wapate riba ya juu zaidi . Serikali ya awamu ya tatu ilijitahidi kukusanya kodi za mapato, ushuru wa forodha na kodi ya ongezeko la thamani mwaka 1995 mamlaka ya kodi TRA ilikuwa inakusanya Tshs 30 bilioni kwa mwezi lakini baada ya kuongeza bidiii ya kusimamia makusanyo ya kodi alipofika mwaka 2000 makusanyo ya kodi kwa mwezi yalifika Tshs 156 bilioni na hii imeongezeka hadi zaidi ya Tshs 260 bilioni kwa mwezi katika awamu ya nne. Kuongezeka kwa makusanyo ya kodi kulikuwa na faida mbili muhimu. Serikali iliweza kupunguza nakisi ya bajeti ya serekali na hivyo kupunguza kiwango cha fedha ambazo serikali hukopa kutoka kwa mabenki na hasa Benki Kuu. Ukopaji huu wa serikali ukiwa wa kiwango cha juu sana huchangia mfumko wa bei kwa ajili ya kuongezeka kwa mzunguko wa fedha wakati uzalishaji wa bidhaa huwa haungezeki. Mapato ya ndani ya serikali yakiongezeka ukopaji kutoka nchi za nje hupungua la muhimu zaidi ni kwamba uwezo wa kulipa madeni ya wafadhili huongezeka na matokeo yake ni kupata misamaha ya madeni kwa nchi maskini kama Tanzania katika mpango wa HIPC na nchi inakuwa inaaminika na wafadhili kwa kuwa inaonekana inaweza kukopesheka. Serikali iliongeza nidhamu katika matumizi ya fedha za serikali na kupunguza ujazi au ongezeko la fedha kutoka Benki Kuu `money supply` kufuatana na sera ya fedha ya kubana ongezeko la fedha katika uchumi kufikia asilimia 10 - 12 kwa mwaka. Kwa kutumia mikakati kama kuuza dhamana za serikali fedha za ziada katika uchumi (excess liqudity) hupungua na hiki ndicho kinachosaidia kupunguza mfumuko wa bei. Mwaka 1995 mfumuko wa bei ulikuwa asilimia 30 lakini kufikia mwaka 2002 mfumuko wa bei ulipungua hadi kufika asilimia tano na hadi sasa mfumko wa bei umefikia asilimia 4.4. Hii ina maana bila kuongeza mishahara au mapato mengine kwa wananchi kwa fedha zile zile kwa mwezi kama mapato kushuka kwa mfumko wa bei kunawawezesha walaji kununua bidhaa nyingi zaidi. Bidhaa hizi ni pamoja na vyakula, nguo, viatu na bidhaa za ngozi, gharama za usafiri, bidhaa za ndani kama radio na TV, gharama za burudani na kwa ujumla bidhaa zote za mlaji. Wananchi na kawaida hufaidika na kushuka kwa mfumuko wa bei kwa sababu matumizi ya mwananchi wa kawaida kwa chakula ni zaidi ya asilimia 64% ya mshahara au mapato kwa mwezi ya mwananchi. Kuimarika kwa uchumi mkuu au `macro-economic stability` ni pamoja na ongezeko dogo la bei za bidhaa zote kwa jumla, ubadilishaji wa fedha za kigeni usiobadilika mara kwa mara na vile vile riba za mabenki zinatabirika. Wataalam wa uchumi wanasema kwamba kudhibiti mfumuko wa bei huvutia wawekezaji wa nje na ndani ya nchi kwa sababu inakuwa rahisi zaidi kwa wawekezaji kupanga mpango yao ya biashara. Hii ni pamoja na kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji kama kuwa na vivutio vya misamaha ya baadhi ya kodi kwa wawekezaji, uboreshaji wa miundo mbinu, utawala bora na kupiga vita rushwa . Kati ya mwaka 1995 uwekezaji kutoka nje umeongezeka kutoka dola za kimarekani milioni kumi kwa mwaka hadi kufikia dola 350 mnamo mwaka 2004 na juhudi zikifanywa kuvutia uwekezaji kuna uwezo wa kuongezeka kwa uwekezaji hadi kufikia dola 500 milioni kwa mwaka katika kipindi kifupi kijacho na haya yamewezekana kwa kuimarisha uchumi mkuu na hasa kuthibiti mfumuko wa bei. Matokeo ya ongezeko la uwekezaji ni pamoja na kuongeza bidhaa zinazozalishwa soko la ndani kwa bei nafuu na ukuzaji wa ajira na fursa nyingi za kuongeza mapato kwa waajiriwa na wale wanaotoa bidhaa huduma kwa wawekezaji kama sekta ya viwanda na madini. Wakulima wa pamba wanapata soko la ndani kama viwanda vingi vya nguo vikianzishwa. Hivi ni kweli kwa malighafi zote zinazozalishwa katika sekta ya kilimo na kufugwa kwa viwanda vipya vinavyoanzishwa. Lakini watanzania hawategemewi kula uchumi mkuu ulioimarika au `macro-economic Stability. Kuimarika kwa uchumi ni lazima kusaidie ukuaji wa sekta mbalimbali za uchumi na shughuli za kibiashara, viwanda na uzalishaji kwa wawekezaji au micro-economic units.Ukuaji wa uchumi ukawa chini ya . asilimia 4.4 mwaka 1995 na sekta nyingine zikawa hazikui kabisa hasa viwanda ambavyo vilidumazwa na sera mbalimbali ikiwepo kulengeza masharti ya biashara ambapo bidhaa nyingi ziliangizwa kutoka nje ya nchi kwa bei nafuu na hivyo bidhaa za ndani kukosa soko. Kuwa na sera nzuri za biashara, viwanda, madini na utalii kumeongeza uzalishaji katika sekta hizi. sekta ya madini sasa inakuwa kwa asilimia 17 na kuchangia asilimia nne katika pato la Taifa. Sekta ya viwanda inakua kwa asilimia 8.4 na kuchangia asilimia katika pato la taifa. Vilevile sekta ya utalii imekuwa ukifanya vizuri kwa ukuaji wa asilimia 12 na kuchangia asilimia 16 katika pato la taifa na kupata shilingi bilioni 600 fedha za kigeni ikiwa nyuma ya kilimo na madini katika kukuza akiba ya fedha za kigeni. Ili wananchi wanufaike kwa ukuaji wa uchumi kuna umuhimu katika maisha yao kuwa bora zaidi kwa kupunguza umaskini. Ndiyo maana serikali ikabuni MKUKUTA kama sera ya ukuaji uchumi na upunguzaji umaskini. Bajeti kubwa ya serikali inaelekezwa katika sekta za elimu, afya, barabara za vijijini na mapambano zidi ya HIV-Aids, Malaria, TB na magonjwa mengine. Kuimarika kwa uchumi ni lazima kuwezeshe wananchi wengi zaidi kupata huduma za jamii na za kiuchumi. Tanzania ni nchi maskani ambayo asilimia hamsini ya watu wake huushi kwa matumizi ya chini ya dola moja ya kimarekani kwa siku. Hivyo sera ya uwezeshaji, na sera ya kurasimisha mali na biashara katika sekta isiyo rasmi ina lengo la kuongeza ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini. Watalaam wa uchumi wa mashirika ya kimataifa ya fedha na wa hapa nchini wanaamini kuwa kama uchumi ikikua kwa asilimia 8 hadi 10 lengo la kupunguza umaskini litafikiwa. Tanzania ni moja wapo ya nchi ambazo zilitia saini mwaka 1999 kufikia malengo ya milenia (millenum Development Goals) Kuna kila dalili kwa Tanzania itafika baadhi ya malengo hayo ifikapo mwaka 2015 kama uchumi utaendelea kuimarika. Malengo hayo ni kupunguza umaskini wa kipato kwa nusu ifikapo mwaka 2015. Lengo jingine ni kila mtoto anayefika umri wa kwenda shule aingie shule za msingi au (Universal Primary Education) na lengo hili limefikiwa zaidi ya asilimia 90. Malengo mengine ni kupambana na maradhi kama VVU?Ukimwi, TB na Malaria. Kupunguza umaskini ni pamoja na kuondoa njaa na kuongezeka kwa lishe kwa watu walio wengi nchini. Melengo mengine ya milenia ni pamoja na kupunguza vifo vya kina mama wazazi, na vifo vya watoto chini ya miaka mitano malengo mengine ni kuwawezesha akina mama kiuchumi na kuboresha mazingira kwa kuwa na maendeleo endelevu au environmental sustainability` lengo lingine ni kukuza ushirikiano na mataifa mengine katika maendeleo. Kukua kwa uchumi ni lazima kuendane na kupunguza tofauti kati ya wananchi wenye vipato vya juu na wale wenye kipato cha chini. sera za MKURABITA, MKUKUTA vitaweza Tanzania ukuze uchumi na kuongeza fursa za uchumi kwa watu wake wengi au wanavyosema watalaam ?economic groth with social justice. Ukuaji wa uchumi ni lazima ulete maendeleo ya kiuchumi na huduma za jamii kwa sababu kama Mwalimu J. Nyerere alivyokuwa akasema maendeleo ni lazima yaboreshe maisha ya watu. Hivyo ukuaji wa uchumi ni lazima ulete maisha bora kwa Watanzania wote ambalo ni lengo kuu la awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Sunday, March 11, 2007

NDIVYO ILIVYO NA HAIBADILIKI TUNAISHI.

Hayo ni maneno yaliyozungumzwa na wanandugu wa baba na mama mmoja. Inakuwa vigumu na anaendelea kuniwia vigumu kuvumilia kisa cha dada na kaka kuishi pamoja kama mke na mume na kuzaa watoto.
Ni familia moja ya kitajiri ambayo wazazi wao walitengana na kugawna watoto.
baba alichukua mtoto wa kiume na mama akamchukua binti yake.
Katika makuzi ya watoto hao hawawahi kujuana kuwa ni ndugu kutokana na kila mmoja wao kulelewa na mzazi mmoja na kufichwa juu ya mwenzie. usemi wa hakuna siri duniani unasimama pale wanandugu hao wanapokutana na damu zao kuvutana kiasi cha kila mmoja kuwa na hisia za kimapenzi kwa mwenzie.
Hawakuficha hisia zao, kila mmoja aliweka bayana ajisikiavyo kwa mwenziwake. wmisho wa yote waliamua kuishi kama mtu na mpenziwake na wakazaa watoto wanne.
mtihani unakuja pale ambapo wanagundua kuwa ni damu moja na jamii kuwataka watengane. hilo limekuwa gumu na kwao halitowezekana kwani kwa sasa wanafanya taratibu za kufunga ndoa. wao wenyewe wanasema wanapendana na hawawezi kuachana.
kama ni makosa wao kukutana na kuwa wapenzi si kosa lao bali ni la wazazi wao ambao walishindwa kuwakutanisha mapema.
matatizo hayo hutokea mara nyingi pale familia zinapokorogana.
lamsingi ni kwamba wanandoa wanaposhindwana , wasiwatenganishe watoto ili kukwepa majanga kama hayo ya mtu na dadake wa kuzaliwa tena baba na mama mmoja wanaishi kma mke na mume na tayari wanawatoto.
Ndivyo Dunia ilivyo hivyoo.